Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2019-02-05

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya kilichopo Kata ya Ilemba katika Halmashauri ya Sumbawanga?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuboresha huduma za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla, Serikali inaendelea na ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya saba kwa gharama ya shilingi bilioni 3.3 ikiwemo Kituo cha Afya Milepa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Vilevile Serikali imeweka kipaumbele cha kujenga hospitali tatu za Halmashauri katika Halmashauri tatu za Wilaya ambazo ni Sumbawanga, Nkasi na Kalambo kwa jumla ya shilingi bilioni 1.5 kila moja na fedha hizo zimepelekwa kwenye Halmashauri husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina vituo vya kutolea huduma za afya saba, viwili vikiwa binafsi na vitano vya Serikali vinavyohudumia watu takribani 369,471. Ujenzi wa Kituo cha Afya Ilemba ulianza mwaka 2011 kwa kujenga Jengo la OPD na nyumba mbili za watumishi kwa kushirikisha wananchi. Mpaka sasa majengo hayo yamefikia hatua ya upauaji na kiasi cha Sh.82,805,611 ambapo ruzuku kutoka Serikali Kuu ni Sh.54,116,121 na nguvu za wananchi Sh.28,789,490 imetumika. Halmashauri inaelekezwa kuzingatia na kuweka kipaumbele kwenye bajeti kuhusu ukamilishaji wa mradi huo kabla ya kuanzisha miradi mipya.