Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 48 2019-02-01

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA aliuliza:-

Kituo cha Polisi Chwaka na Kituo cha Polisi Jozani vina tatizo kubwa la gari la kufanyia doria na ulinzi:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa magari mawili kwa Vituo hivyo katika bajeti ya 2018/2019?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bhagwanji Maganlal Meisuria, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi Chwaka na Kituo cha Polisi Jozani vipo katika Mkoa wa Kusini Unguja. Tayari Mkoa wa Kusini Unguja umeshapatiwa magari mawili aina ya Ashock Leyland – Trooper na Sauvana kwa ajili ya kusaidia utendaji kazi wa Polisi Mkoani humo ikiwemo doria.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi bado linaendelea kupokea magari mapya kupitia mkataba wa magari 777 kutoka Kampuni ya Ashock Leyland Limited ya India. Hivyo kutokana na hitajio kubwa la rasilimali ya magari lililopo katika mikoa yote ikiwemo Mkoa wa Kusini Unguja na Jimbo la Chwaka, Jeshi la Polisi litaendelea kugawa magari katika mikoa kwa kadri magari yatakavyopatikana na kwa kuzingatia vipaumbele ambavyo ni kiwango cha uhalifu katika maeneo husika na ukubwa wa maeneo ya doria.