Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 13 2019-01-30

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-

Serikali imeanzisha sera nzuri ya viwanda nchini ili kukuza uchumi wa viwanda na maendeleo kwa wananchi.

(a) Je, Serikali haioni upungufu wa mafundi mchundo na mafundi sadifu kuwa ni kikwazo cha ufanisi wa sera ya viwanda?

(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuziimarisha shule za ufundi za Moshi, Ifunda, Tanga na Mtwara ili kuwaandaa na kuwapatia mafundi sadifu kufanikisha sera ya viwanda nchini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa mafundi mchundo (technicians)na mafundi stadi (artisans)katika kutekeleza azma ya Serikali ikifikia uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo mwaka 2025. Hadi kufikia Desemba 2018, kulikuwa na vyuo vya ufundi stadi 449 nchini ambavyo vilidahili wanafunzi 119,184 kujiunga katika fani mbalimbali za ufundi ili kuwa na wataalam wa kutosha kuendana na mageuzi ya viwanda nchini. Vilevile, kupitia programu ya taifa ya kukuza ujuzi kwa vijana, jumla ya vijana 10,858 wamefaidika na mafunzo mbalimbali ya ujuzi katika fani za useremala, uashi, terazo, uchongaji vipuri, ufundi umeme, ufundi bomba, uchomeleaji, ushonaji, upishi, huduma za hoteli, ufundi magari na kutengeneza viatu vya ngozi. Mikakati hiyo inakusudia kuwa na wataalam wa kutosha ili kufanikisha utekelezaji wa sera ya viwanda.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutekeleza mkakati wa kuborsha mazingira ya elimu nchini ikiwemo ukarabati wa shule na miundombinu ambapo kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) kati ya mwaka wa fedha 2015/2016 hadi Desemba, 2018 Serikali imetumia jumla ya shilingi bilioni 11.2 kwa ajili ya ukarabati wa shule kongwe za ufundi. Shule zilizokarabatiwa ni shule ya Sekondari Moshi kwa shilingi bilioni 2, Ifunda shilingi bilioni 2.8, Tanga shilingi bilioni 1.8, Musoma shilingi bilioni 1.2, Bwiru Wavulana shilingi milioni 825 na Iyunga shilingi milioni 978. Lengo la Serikali ni kuhakikisha shule hizo za ufundi zinaimarishwa ili kuwa na wataalam watakaoshiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa viwanda.