Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 40 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 339 2018-05-30

Name

Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. SALUM MWINYI REHANI) aliuliza:-
Kambi za Jeshi za Ubago na Dunga zinawanyanyasa wananchi wa Shehia ya Kidimi kwa kuwataka waondoke katika maeneo hayo ambayo ni ya iliyokuwa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika kwa zaidi ya miaka 40 wameanza kupima na kuweka bikoni:-
Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo na hatma ya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salum Mwinyi Rehani, Mbunge wa Uzini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya Ubago na Dunga yalipimwa mwaka 1985, kwa unyeti wake Uongozi wa Mkoa na Wilaya husika zilishirikishwa. Aidha, taratibu zote za utwaaji ardhi kwa matumizi ya umma zilitumika na kuruhusu maeneo haya kupimwa yaani Ubago na Dunga. Maeneo yote mawili tayari yamejengwa miundombinu ya Kijeshi ambayo siyo rafiki kwa matumizi mengine ya kiraia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Ardhi Na. 12 ya mwaka 1992 ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ilipoanza kutumika, ramani za upimaji wote uliofanyika kabla ya 1992 zilitakiwa kupitiwa upya. Hivyo, ramani za upimaji wa maeneo ya Ubago na Dunga zilikwama kupata Hatimiliki kutokana na sheria hiyo. Hali hii ilitoa mwanya kwa wananchi kuingilia sehemu ya maeneo ya Kambi kwa shughuli za kiraia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 19 Mei, 2018 kulifanyika kikao na ukaguzi wa pamoja kati ya Wizara yangu na Waheshimiwa Mawaziri wa SMZ pamoja na Mkurugenzi wa Mipango Miji na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa Zanzibar kwa lengo la kupata ufumbuzi wa kudumu wa wananchi walioko katika maeneo haya. Ukweli ni kwamba eneo hili linatumiwa na JWTZ kihalali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, timu ya watalaam kutoka Idara ya Ardhi ya SMZ ikishirikiana na Uongozi wa Mkoa na Wilaya husika wanaendelea na zoezi la kufanya tathmini ya uvamizi wa maeneo haya ili hatimaye kusaidia kufikia uamuzi kuhusu hatma ya wananchi ndani ya maeneo haya nyeti ya JWTZ.