Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 197 2018-05-08

Name

Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y MHE. RASHID A. AKBAR) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia Hospitali ya Wilaya ya Newala watumishi pamoja na vifaa tiba?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Ajali Akbar, Mbunge wa Newala Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi kwa kuhakikisha vituo vinakuwa na vifaa tiba vinavyohitajika. Hospitali zinapatiwa rasilimali watu na fedha kwa ajili ya kununua dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali ilitenga kiasi cha shilingi 198,671,475mpaka sasa shilingi 120,510,860 zimepokelewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa. Katika mwaka wa fedha 2018/19 Serikali imetenga shilingi 244,066,959.92 kwa ajili ya vifaa tiba na dawa katika Hospitali ya Wilaya ya Newala.
Mheshimiwa Spika, uhaba wa watumishi ni changamoto inayovikabili vituo vingi vya kutolea huduma za afya nchini. Hata hivyo Serikali inaendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya kadri vibali vya ajira vinavyopatikana. Mwezi Novemba, 2017 Halmashauri ya Mji wa Newala ilipata watumishi 12 wa kada mbalimbali za afya na katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri imeomba kibali cha kuajiri watumishi 60 wa kada mbalimbali za afya. Serikali itaendelea kupeleka watumishi wa afya, vifaa tiba na vitendanishi ili kuboresha huduma za afya katika Wilaya ya Newala.