Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 12 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 98 2016-05-04

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA) aliuliza:-
Majengo mengi ya Mahakama za Mwanzo yamechakaa sana:-
(a)Je, Serikali ina mpango gani wa kuyafanyia ukarabati au kuyajenga upya?
(b)Je, Serikali haioni kama Mahakama ya Mnazi Mmoja - Dar es Salaam imeelemewa na kesi nyingi hivyo iangalie namna ya kupunguza kesi?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inao mpango wa ujenzi na ukarabati wa Mahakama wa miaka mitano 2015 - 2020 na hivi sasa inaufanyia marekebisho ili kukidhi mahitaji sahihi ya wakati husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka 2015/2016, Serikali lilitoa fedha ya kiasi cha shilingi bilioni 12.3 za miradi ya maendeleo sawa na asilimia 100% ya fedha zilizopangwa. Fedha hizo zitatumika katika ujenzi na ukarabati wa Mahakama za Wilaya 12 ambazo ni Mahakama za Bariadi, Kilindi, Kasulu, Kondoa, Bukombe, Makete, Sikonge, Nkasi, Bunda, Chato, Nyasa na Namtumbo. Aidha, fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa Mahakama mpya za mwanzo 10 za Longido (Manyara), Terati (Simanjiro-Manyara), Machame (Hai), Makongolosi (Chunya-Mbeya), Unyankulu (Urambo-Tabora), Sangabuye (Ilemela-Mwanza), Mtowisa (Sumbawanga), Njombe Mjini, Gairo (Morogoro) na Mangaka (Mtwara).
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/2016, itakamilisha ukarabati wa Mahakama Kuu Shinyanga, Mtwara, Tanga na Mbeya. Maandalizi ya utangazaji wa zabuni za ujenzi wa Mahakama Kuu Kigoma na Mahakama Kuu Mara yanaendelea.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali ina mpango wa kujenga Mahakama mpya ya Kinyerezi na Ilala. Hivyo, ni matarajio yangu kuwa kukamilika kwa miradi hii kutawezesha kupunguza mlundikano wa mashauri katika Mahakama ya Mnazi Mmoja.