Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 61 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 510 2018-06-29

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. PHILIPO A. MULUGO aliuliza:-
Je, Serikali haioni haja ya kuipandisha hadhi Hospitali Teule ambayo inamilikiwa na Kanisa Katoliki Dayosisi ya Mbeya iwe Hospitali Teule ya Wilaya ili wananchi wa Songwe waweze kupata huduma stahili?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Philipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Songwe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 2 Januari, 2018, Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ilisaini mkataba na Kanisa Katoliki, Jimbo la Mbeya uliopandisha hadhi ya Hospitali ya Mwambani kuwa Hospitali Teule ya Wilaya ya Songwe. Kufuatia mkataba huo, Serikali imeongezea fedha za ununuzi wa dawa na vifaa tiba kwa hospitali hiyo kutoka shilingi milioni 27.5 kwa mwaka 2017/2018 hadi shilingi milioni 105 kwa mwaka 2018/2019. Mkataba huo utaendelea hadi Serikali itakapokamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Songwe, ambayo katika mwaka wa fedha 2018/2019 imetengewa shilingi milioni 1.5.