Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 59 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 498 2018-06-27

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:-
Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kipaumbele na kutenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe lakini kutokana na ukomo wa bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 bajeti hiyo haikupatikana. Hata hivyo, Serikali imetoa shilingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo viwili vya Afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ambavyo ni Iboya kilichopokea shilingi milioni 400 na Kituo cha Afya Masumbwe kilichopokea shilingi milioni 400 pia.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, katika Mkoa wa Geita, Serikali imeweka kipaumbele na kuanza ujenzi wa Hospitali za Wilaya katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Halmashauri ya Wilaya Nyang’hwale ambapo zimetengwa jumla ya shilingi bilioni tatu.