Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 57 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 486 2018-06-25

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-
Je, ni vigezo vipi ambavyo Serikali imeviweka juu ya kampuni zinazowekeza kwenye michezo nchini kuruhusiwa Ligi husika kubeba majina ya kampuni hizo kama vile Vodacom Premier League badala ya Tanzania Premier League?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kuongezeka kwa gharama za mfumo wa uendeshaji wa Mpira wa Miguu Duniani, Shirikishao la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limelazimika kutafuta wadhamini au wafadhili wa kusaidia kuendesha shughuli za mpira wa miguu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya makubaliano yanayofikiwa kati ya Shirikisho na Wadhamini ni mdhamini kujitangaza kupitia mchezo wenyewe. Kwa mfano, ligi kuu ya Uingereza wakati ikifadhiliwa na Benki ya Backlays, ligi ilijulikana kwa jina la Backlays English Premier League. Hapa Afrika Mashariki kuna mashindano ya Kagame Cup ambayo mfadhili wake ni Rais wa Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame na yanajulikana kama CECAFA Kagame Cup.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo suala la ligi kuu ya Tanzania kutumia jina la Mdhamini wa ligi hiyo, Kampuni ya Vodacom, linatokana na makubaliano ya kimkataba baina ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania na mdhamini wa ligi hiyo ambayo ni kampuni ya Vodacom.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mkataba huo, miongoni mwa masuala waliyokubaliana ni pamoja na mdhamini kuwa na haki ya kutumia jina lake (Naming Right) katika uendeshaji wa ligi hiyo.