Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 54 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 463 2018-06-20

Name

Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHIDI M. CHUACHUA) aliuliza:-
Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Masasi halina nyumba za makazi na usafiri kwa muda mrefu sana:-
a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea askari hao nyumba za kuishi kwa sababu nyumba wanazoishi sasa zimechakaa sana na pia hazitoshelezi mahitaji yao?
b) Je, ni lini Serikali itawapatia usafiri wa uhakika Askari hao ili waweze kusimamia usalama wa raia na mali zao kwa uhakika?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Mohamed Chuachua, Mbunge wa Masasi, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua tatizo la uhaba wa nyumba za makazi kwa Askari wa Jeshi la Polisi nchini ikiwemo Wilaya ya Masasi. Hata hivyo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza tatizo la makazi ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wananchi na wadau kujenga nyumba kwa ajili ya makazi ya Askari.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali itajenga nyumba za kuishi Askari kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, Wilaya ya Masasi ina magari matatu ambapo kati ya hayo magari mawili ni mabovu. Jeshi la Polisi hugawa magari kwa kuzingatia vigezo mbalimbali ikiwemo hali ya uhalifu, sababu za kiutawala na jiografia ya mahali husika. Kwa kuzingatia vigezo hivyo hususani jiografia yake, Wilaya ya Masasi itapewa kipaumbele katika mgao wa magari mara yatakapopatikana.