Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 53 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 450 2018-06-19

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:-
Sekta ya utalii inachangia pato kubwa la fedha za kigeni katika nchi yetu.
Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara ya Serengeti ambayo ni mbovu kiasi cha kufanya watalii kukataa kupita huko?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Alexander Mahawe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa naibu Spika, Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ndiyo zinachangia zaidi katika mapato ya fedha za kigeni zitokanazo na shunguli za utalii hapa nchini. Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ina ukubwa wa kilometa za mraba 14,763 na barabara zenye urefu wa kilometa 3,155. Barabara hizo ni pamoja na barabara kuu zinazounganisha Hifadhi na Mikoa ya Arusha, Mara na Simiyu. Barabara nyingine ni zile za mizunguko ya utalii na nyingine ni za utawala na doria. Barabara zote hizo ni za kiwango cha changarawe.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zenye matumizi makubwa ni zile kuanzia mpaka unaotenganisha Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro hadi Kituo cha Seronera yenye urefu wa kilometa 60 na kilometa 30 kutoka Seronera hadi lango na Ikoma. Barabara hizi wakati wa msimu wa watalii wengi zinatumiwa na magari zaidi ya 300 kwa siku. Kutokana na matumizi makubwa kiasi hicho, barabara hiyo yenye kiwango cha changarawe uchakavu wake huongezeka kwa kasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwezi Agosti, 2016 hifadhi inaendelea kuelekeza nguvu za ziada kuhudumia barabara hizi wakati wote wa msimu wa watalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, juhudi zinazoendelea zinahusisha kufanya matengenezo ya barabara hizo kwa kutumia nyenzo mbalimbali ikiwemo mitambo miwili ya barabara yaani motor graders pamoja na malori. Ili kupata ufumbuzi wa muda mrefu kukabiliana na changamoto hiyo ya ubovu wa barabara, Shirika la Hifadhi za Taifa linaendelea kutafuta teknolojia mbadala ili kuwa na barabara zitakazodumu bila kuathiri ikolojia ya wanyamapori.