Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 94 2016-05-04

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:-
Sumbawanga ina Wilaya mbili ambazo ni Sumbawanga Mjini na Sumbawanga Vijijini:-
Je, kwa nini ina Mkuu wa Wilaya mmoja?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa Halmashauri mbili unatokana na Sheria za Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sura 287 (Mamlaka za Wilaya) na Sura 288 (Mamlaka ya Miji) ambapo lengo ni kusogeza huduma karibu na wananchi. Sheria hizi zinampa mamlaka Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa kuanzisha Halmashauri katika Wilaya moja zenye hadhi ya Wilaya, Mji, Manispaa na Jiji. Aidha, Wilaya ni sehemu ya Serikali Kuu ambayo uanzishwaji wake unazingatia Sheria ya Uanzishwaji wa Maeneo Mapya kwa maana ya Mikoa na Wilaya, Sura 297 ya mwaka 2002.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili Wilaya mpya iweze kuanzishwa vipo vigezo na taratibu mbalimbali ambazo vinapaswa kuzingatiwa ikiwa ni pamoja na mapendekezo hayo kujadiliwa katika Mikutano ya Vijiji, Baraza la Madiwani, Kamati za Ushauri za Wilaya na Mikoa. Hivyo, endapo halmashauri hizo mbili zikikidhi vigezo na kuwa na Wilaya kiutawala na hivyo kuwa na Mkuu wa Wilaya, nashauri mapendekezo hayo yapitishwe katika vikao vya kisheria ili yaweze kujadiliwa na hatimaye yawasilishwe kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kwa hatua zaidi kwa mujibu wa sheria.