Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 52 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 440 2018-06-18

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. . JOSEPH R.SELASINI - (K.n.y MHE. RUTH H. MOLLEL) aliuliza:-
Serikali ya Awamu ya Tano inajinasibu kuzingati Utawala wa Sheria, Kanuni na taratibu katika Utumishi wa Umma. Hata hivyo, kuna ushahidi kuwa baadhi ya viongozi wanakiuka maadili na taratibu lakini wameachwa pasipo kuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu:-
(a) Je, tunaweza kujenga uchumi imara bila Watumishi wa Umma kuzingatia Kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma?
(b) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Taifa linadumisha umoja ulioasisiwa na Baba wa Taifa?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Hiyob Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, napenda kusisitiza kuwa nchi yetu inaongozwa kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu zinazojumuisha zile zinazosimamia Utumishi wa Umma. Endapo wapo watu wanaokiuka sheria, hao wanafanya hivyo kutokana na upungufu wao na kamwe haiwezi kutafsiriwa kuwa ni Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano kwenda kinyume cha sheria.
Mheshimiwa Spika, hatua hizi za kinidhamu huchukuliwa pale inapothibitika pasipo shaka yoyote kuwa kosa limetendeka kwa makusudi. Pale ilipogundulika kuwa utendaji usiozingatia sheria unatokana na kutoelewa misingi ya Sheria, Serikali imelazimika kutoa mafunzo maalum ili kuwajengea uwezo watendaji wake ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi.
(b) Mheshimiwa Spika, napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kuwa Umoja wa Tanzania ulioasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shekhe Abeid Aman Karume unaendelezwa kwa njia mbalimbali, ikiwemo kuadhimisha siku maalum za viongozi hawa, ambapo maoni yao huakisiwa kupitia mikutano ya hadhara na makongamano mbalimbali kwa lengo la kuenzi malengo yao.