Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 438 2018-06-18

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya kuwahudumia wagonjwa katika kituo cha Afya cha Magunguli –Mgololo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Menrald Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, gari la wagonjwa kwa ajili ya Kituo cha Afya Magungulu - Mgololo kilichopo kata ya Magungulu imekwishapatikana. Gari hili lilitolewa na Mheshimiwa Rais wakati anatoa msaada wa magari ya wagonjwa kwa halmashauri mbalimbali hapa nchini mnamo mwezi Machi, 2018 na taratibu za usajili zinaendelea.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa kutambua uhitaji wa gari katika kituo hiki, gari hili limepelekwa kituoni moja kwa moja na kuanza kutumika huku taratibu za usajili wake zikiwa zinaendelea. Ni matumaini yetu kuwa gari hili, litasaidia kuleta wepesi kwa wananchi kufikia huduma za afya pale mahitaji yatakapo yanajitokeza.