Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 50 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 429 2018-06-13

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi.
• Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi pamoja na nyumba za askari zitajengwa?
• Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya Mbeya?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo:-
i. Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ni miongoni mwa Wilaya Mpya za Kipolisi zilizoanzishwa hivi karibuni. Jeshi la Polisi kwa kutambua ukosefu wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya pamoja na nyumba za makazi ya askari linashirikiana na wananchi na wadau mbalimbali kujenga jengo la Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ambalo linajumuisha Kituo cha Polisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa jengo hili umefikia hatua ya umaliziaji na changamoto iliyobaki ni ujenzi wa nyumba za kuishi askari.
ii. Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari matatu ambapo gari moja ni chakavu linahitaji matengenezo ili liweze kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya vituo vya Polisi katika Halmashauri ya Mbeya pamoja na kwingineko nchini kwa awamu kwa kutegemea rasilimali zilizopo na upatikanaji wa fedha.