Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 416 2018-06-12

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:-
Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika kampeni za uchaguzi tarehe 18 Novemba, 2005 aliwaahidi wananchi wa Kibiti kuwa Serikali yake itajenga barabara ya Kibiti-Kikale ili kupunguza adha kubwa ya usafiri wanayopata wananchi wa Vijiji vya Mchukwi, Rungungu, Nyamatanga na Kikale ambamo barabara hiyo inapita:-
a) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?
b) Je, ujenzi huo unaotarajiwa utakuwa ni wa kiwango gani?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali ya Mheshimiwa Ally Seif Ungando, Mbunge wa Kibiti, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kibiti - Kilale ni sehemu ya barabara ya Kingwira – Ruaruke - Mtunda – Myuyu yenye urefu wa kilometa 66.2 ambapo kipande cha Kibiti - Kikale kipo kati ya barabara ya Ruaruke - Mtunda. Tangu kutolewa kwa ahadi na Mheshimiwa Rais mwaka 2005 barabara hiyo imefanyiwa matengenezo ya kilomita 56 na ukarabati wa daraja la Ruhoi lenye urefu wa mita 24 kwa gharama ya shilingi milioni 151.6.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2018/2019, barabara hiyo imetengewa shilingi milioni 185.02 kupitia TARURA kwa ajili ya matengenezo ya kilomita 65.9 kwa kiwango cha changarawe ili kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa eneo hilo.