Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 47 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 401 2018-06-08

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO) aliuliza:-
Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha maendeleo ya michezo mbalimbali lakini sheria inayosimamia michezo ya mwaka 1967 ina upungufu makubwa sana.
(a) Je, kwa nini Serikali haijatunga sheria mpya ya michezo ambayo itakwenda sambamba na mahitaji ya jamii kwa sasa?
(b) Je, kwa nini Serikali haina bajeti kwa ajili ya Timu za Taifa zinazobeba bendera kwa ajili ya kuitangaza nchi Kimataifa?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba kwa ridhaa yako kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ndumbaro nitoe pongezi kwa Mabingwa wa Ligi ya Tanzania Bara Simba, kwa kufanikiwa kutinga fainali ya michuano ya Sport Pesa Super Cup nchini Kenya. Simba wamethibitisha kuwa hawakupata ubingwa wa Tanzania Bara kwa kubahatisha, bali kwa soka la viwango na sasa wanaingia fainali kupambana na mabingwa wa Kenya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, Mbunge wa Songea Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iko katika hatua za mwisho kabisa kukamilisha maboresho ya sera ya michezo ya mwaka 1995 na sera mpya tutakayoipitisha ndani ya mwaka huu, itakuwa msingi wa sheria mpya ya michezo nchini.
b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya michezo nchini ambayo inaendana na ukubwa wa mashindano yanayotukabili. Kwa mfano, mwakani Tanzania ni mwenyeji wa mashindano ya AFCON ya mpira wa miguu kwa vijana chini ya umri wa miaka 17. Hivyo, mbali na vyanzo vingine vya fedha, Bunge hili tukutu limeidhinisha shilingi bilioni moja itumike kuboresha miundombinu ya Kiwanja cha Taifa na Kiwanja cha Uhuru na shilingi 293,619,000 kwa maandalizi mengine yanayohusiana na AFCON.