Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 47 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 400 2018-06-08

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE (K.n.y. MHE. DANIEL NSANZUGWANKO) aliuliza:-
Mkoa wa Kigoma hususan Wilaya za Kasulu na Kibondo zimekuwa makazi ya wakimbizi kwa muda mrefu sana.
Je, ni lini Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na UNHCR itakuja na mpango kabambe wa kusaidia maeneo yaliyoathiriwa na ujio wa wakimbizi hao (a comprehensive plan and support for refugee affected areas)?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Nicodemus Nsanzugwanko, Mbunge wa Kasulu Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli baadhi ya maeneo ambayo hupokea wakimbizi nchini hupata athari mbalimbali ikiwemo uharibifu wa mazingira. Hata hivyo, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) inatekeleza mipango mbalimbali inayolenga kuboresha huduma kwenye jamii katika Wilaya zinazohifadhi wakimbizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Wilaya za Kibondo na Kasulu huduma ambazo zimekuwa zikiboreshwa ni pamoja na afya, elimu, kilimo, masoko, ujasiriamali pamoja na hifadhi ya mazingira.