Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 373 2018-06-05

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunga mkono wananchi wa Kata ya Haneti kwa kumalizia ujenzi wa chumba cha upasuaji ambacho kilianzishwa kwa nguvu za wananchi na Mfuko wa Jimbo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatoa pongezi kwa wananchi wa Kata ya Haneti pamoja na Mbunge wao Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga kwa juhudi kubwa za kuibua na kuanza ujenzi wa chumba cha upasuaji kwa ajili ya kuokoa maisha ya wananchi hususani akina mama na watoto. Ujenzi huo umefikia hatua ya kufunika jamvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali kuboresha miradi kupitia fedha za miradi ya maendeleo na kuchagua miradi michache itakayotoa matokeo ya haraka, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino katika mwaka wa fedha 2017/2018 ilitengewa shilingi milioni 350 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha upasuaji katika Kituo cha Afya cha Haneti na shilingi 350 kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mlowa Barabarani. Ujenzi huo utakamilishwa baada ya fedha hizo kupokelewa kutoka Hazina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa majengo haya ya upasuaji yatakapokamilika kwa kiasi kikubwa yatawezesha kuboreshwa kwa huduma za akinamama wajawazito pamoja na kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vitokanavyo na uzazi.