Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 118 2018-09-14

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-
Kata za Gare, Kwai, Kwemashai, Makanya, Kilole, Ngwelo na Ubiri hazikufikiwa na REA III mpaka sasa:- Je, ni lini sasa Serikali itafikisha umeme kwenye kata hizo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alhaji Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza Miradi ya Kupeleka Miradi ya Umeme Vijijini kupitia Wakala wa Nishati (REA). Mradi wa REA III mzunguko wa kwanza ulianza Julai, 2017. Vijiji vitakavyopelekewa umeme kwenye Jimbo la Lushoto ni pamoja na Magamba, Kwegole, Kwehungulu, Kwebarabara, Maboi, Milemeleni, Kungului, Shume A, Makunguru, Shume B, Ngazi, Mhezi, Kwezindo, Kweboi, Nkelei, Viti, Langoni B, Vuli A na Kwemakulo, Mradi huu unatarajiwa kukamilika Juni, 2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya mradi huu zinahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 5.67, njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 46, ufungaji wa transfoma 23 za 50 kVA pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 520. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 1.9.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji vya Kata ya Gare, Kwai, Kwemashai, Makanya, Kilole, Ngwelo na Ubiri vitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili wa mradi wa REA III utakaoanza Julai, 2019 na kukamilika Juni, 2021. Ahsante.