Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 8 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 104 2018-09-13

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. ANDREW J. CHENGE (K.n.y. MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta baadhi ya sheria zilizopitwa na wakati Bungeni ili ziweze kupitiwa upya ziendane na wakati uliopo hasa zikiwemo Sheria za Usalama Barabarani?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. ANTHONY P. MAVUNDE K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Wilfred Kikwembe, Mbunge wa Kavuu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa sheria za nchi zinakidhi mahitaji ya wakati, Serikali imekuwa ikifanya mapitio ya sheria ya kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania iliyopo chini ya Wizara ya Katiba na Sheria.
Mheshimiwa Spika, Tume hii imekuwa ikifanya mapitio na tafiti mbalimbali ambazo zimekuwa ni msingi wa marekebisho ya sheria au kutungwa kwa sheria mpya hapa nchini. Kazi ya mapitio ya sheria ni endelevu na Serikali itaendelea kuwasilisha Bungeni miswada ya sheria ambayo inalenga kurekebisha sheria za nchi au kutunga sheria mpya ili kukidhi matakwa ya wakati.