Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 98 2018-09-13

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA (K.n.y. MHE. BONIPHACE M. GETERE) aliuliza:-
Serikali imekuwa na mpango wa kufanya maboresho ya Vituo vya Afya nchini na Kituo cha Afya cha Ikizu ambacho kinahudumia kata zaidi ya 13, majengo yake licha ya kuwa hayatoshelezi hasa wodi ya akina mama wajawazito na watoto, lakini pia yamechakaa sana.
Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu maboresho ya kituo hicho?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Bunda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Ikizu ni kati ya vituo viwili vinavyotoa huduma za upasuaji katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, kituo kingine ni Kasahunga. Katika kukiboresha Kituo cha Afya Ikizu ili kuweza kutoa huduma bora Serikali imeendelea kufanya maboresho ya miundombinu kwa awamu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali ilifanya ukarabati wa wodi ya wazazi kwa gharama ya shilingi milioni 20. Vilevile katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imepeleka kiasi cha shilingi milioni 33.5 fedha za ufadhili wa AGPAHI kwa ajili ya ukarabati wa jengo la kutolea huduma na tiba na jengo la stoo. Aidha, Halmashauri imetoa kiasi cha shilingi milioni 5.98 kwa ajili ya kusimika mfumo wa kukusanya mapato na takwimu za afya ili kukiwezesha kudhibiti upotevu wa mapato. Serikali inaendelea kutenga fedha kukikarabati kituo hiki ili kuboresha miundombinu na utoaji wa huduma kwa wananchi.