Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 97 2018-09-12

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi walio kwenye vijiji vilivyopo kwenye mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa kuwarahisishia upatikanaji wa vitabu vya usajili Wilayani?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA YA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba tano ya mwaka 1999 kifungu la 21 na Kanuni ya 36, kila kijiji chenye mpango wa matumizi bora kwa ardhi inapaswa kuwa na daftari la usajili wa ardhi ambalo linatunzwa na Afisa Mtendaji wa Kijiji. Daftari la usajili ni daftari ambalo hutumika kusajili hati za hakimiliki za kimila zinazotolewa katika ardhi ya kijiji husika. Utoaji wa hatimiliki za kimila hutanguliwa na zoezi la uandaaji wa mpango wa matumizi ya ardhi ambayo inalenga kuboresha mipango ya matumizi ya ardhi katika kijiji kwa kuondoa mgongano wa matumizi katika ardhi za vijiji pamoja na kuiongezea thamani ardhi hiyo kuifanya kuwa ni mtaji hai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwepo na changamoto za upatikanaji wa madaftari ya usajili wa ardhi katika baadhi ya Halmashauri kutokana na uhaba wa rasilimali fedha kwa ajili ya kuchapisha madaftari hayo. Katika kutatua changamoto hiyo, Wizara imekuwa ikisadiana na Halmashauri kuzipatia madaftari ya usajili wa ardhi wakati wa kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi. Hata hivyo, Wizara imeanza kutoa hati za hakimiliki za kimila kwa kutumia mfumo wa kielektroniki katika Wilaya ya Kilombero, Ulanga, Malinyi, Mkoani Morogoro. Teknolijia hii itakapoenea katika maeneo yote nchini itaondoa kabisa mahitaji ya madaftari ya usajili wa ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninahimiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa zinatenga fedha katika bajeti zao kwa ajili ya kuchapisha madaftari ya usajili wa ardhi wakati tunasubiri teknolojia ya utaji wa Hatimiliki za kimila kwa njia ya kielektroniki kuenea katika nchi nzima.