Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 76 2018-09-11

Name

Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA aliuliza:-
Serikali inamhudumia Faru Fausta kwa gharama ya shilingi milioni 64 kwa mwezi na ambae hazalishi kutokana na kuwa ni mzee sana lakini Serikali hiyo haiwezi kumhudumia mwananchi aliyezeeka ambae hawezi kufanya shughuli zozote za kujikimu maisha na hana mtu wa kumsaidia.
Je, ni kipi kilicho muhimu zaidi kwa Serikali kati ya Faru Fausta au mwananchi mzee asiyeweza kufanya lolote na hana wa kumsaidia?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suzana Chogisasi Mgonukulima, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Faru Fausta amekuwepo eneo la Hifadhi ya Ngorongoro tangu mwaka 1965. Kwa sasa Faru huyu ndiyo mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani. Kutokana na uadimu wa wanyama hao, uwepo wa Faru Fausta umekuwa kivutio kikubwa kwa watalii na watafiti wa ndani na nje ya nchi na hivyo kuchangia kwa kiwango kikubwa mapato ya hifadhi ya Ngorongoro na Serikali kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uzee, Faru Fausta alijeruhiwa na fisi tarehe 9 Septemba, 2016 hivyo kulazimisha atunzwe kwenye kizimba (cage) kwa ajili ya uangalizi maalum ambao unahusisha matibabu, chakula na ulinzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama kubwa iliyokuwepo kipindi ikilichopita ilitokana na hali ya dharura iliyohitajika ikiwemo miundoimbinu, ulinzi, matibabu na malisho maalum ambapo matumizi kwa mwezi yalikuwa ni takribani shilingi 1,435,571. Kwa sasa afya ya Faru Fausta inazidi kuimarika kadri siku zinavyozidi kwenda hivyo gharama za uangalizi zimeshuka hadi kufikia shilingi 285,000 kwa mwezi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo Faru Fausta si kwamba ni muhimu kuliko binadamu wazee bali uamuzi wa kumtunza kwenye kizimba ulifanyika kwa lengo la kunusuru maisha yake ili hatimaye aendelee kuwa kivutio cha utalii na kuingiza fedha za kigeni nchini. Fedha zote hizo zinaingia kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali.