Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 62 2018-09-10

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA (K.n.y. MHE. BUPE MWAKANG’ATA) aliuliza:-
Vijana wengi wamejiajiri katika shughuli mbalimbali ikiwemo waendesha bodaboda, lakini waendesha bodaboda hao wamekuwa wakisumbuliwa sana na askari wa barabarani kwa kutozwa faini ambazo muda mwingine hazina maana na hivyo kuwakatisha tamaa.
Je, Serikali inachukua hatua gani ili kudhibiti vijana hawa wasinyanyaswe?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mchango mkubwa wa biashara ya pikipiki kwa huduma ya usafiri kwa jamii ambapo vijana wengi wamepata ajira hivyo kukuza kipato chao. Umuhimu mkubwa wa usafiri huu hauwaondolei wahusika wa usafiri huu wajibu wa kuzingatia Sheria na Kanuni za Usalama Barabarani ili kuufanya usafiri huu kuwa salama kwa watumiaji.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba Jeshi la Polisi litaendelea kuwachukulia hatua wale wote ambao wanakiuka Sheria na Kanuni za usalama barabarani, ni rai yangu kwa wale wote ambao wanahisi kuonewa ama kunyanyaswa wakati wakitumia usafiri huu kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ama Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.