Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 11 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 86 2016-05-03

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA aliuliza:-
Baadhi ya Kambi za Jeshi la Wananchi nchini (JWTZ) zina majengo chakavu sana ikiwemo Kambi ya Nyuki Zanzibar:-
Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi wa Kambi hizi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Msabaha, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kambi za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania zina majengo chakavu ikiwemo Kambi ya Nyuki, Zanzibar. Hali hii imetokana na ukweli kwamba, Kambi nyingi za Jeshi zilirithi majengo yaliyokuwa yanatumiwa na Taasisi nyingine. Hata hivyo, Jeshi lina utaratibu wa kufanyia matengenezo majengo yake mara kwa mara kwa kadri ya upatikanaji wa fedha za bajeti za maendeleo.