Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 55 2018-09-10

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliokumbwa na sakata la vyeti fake?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako kuwa Serikali imeshatoa vibali vya kuajiri watumishi 15,000 ili kuziba pengo lililosababishwa na kuondolewa kwenye orodha ya malipo ya mishahara watumishi wa umma waliobainika kughushi vyeti. Vibali kwa ajili ya watumishi hao vimetolewa katika ngazi ya Wizara, Idara zinazojitegemea, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa na waajiri wote wameendelea kujaza nafasi hizo.
Mheshimiwa Spika, Serikali pia imetoa vibali vya ajira kwa mamlaka zote za Serikali za Mitaa Kumb. Na. CFC.26/ 205/01/PF/91 cha tarehe 22 Agosti, 2017 na kibali kingine cha tarehe 12, Machi, 2018 kuziba nafasi zote za Watendaji wa Vijiji na Mtaa zilizoachwa wazi kutokana na zoezi la kuhakiki vyeti kwa kuajiri watumishi wapya.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa kutambua umuhimu wa kuajiri watumishi wa kada mbalimbali, Serikali imetoa vibali vya kuajiri watumishi 22,150 wakiwemo watumishi wa kada za ualimu 6,840, fundi sanifu wa maabara za shule 160, kada za afya 8,000, wahadhiri wa vyuo vikuu 624 na watumishi 6,526 wa kada nyingine.