Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 26 2018-09-05

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-
Baadhi ya Mahakama za Mwanzo kama vile Matemanga, Napakanya na nyingine nyingi ni chakavu na hazipati fedha kwa ajili ya ukarabati hali inayosababisha Mahakimu na watumishi wengine kufanya kazi katika mazingira magumu sana:-
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa Mahakama hizo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Yassin Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana kabisa na Mheshimiwa Mbunge kuwa kwa baadhi ya maeneo watumishi wetu wanafanya kazi katika mazingira magumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Tunduru ina jumla ya Mahakama za Mwanzo tisa ambazo karibu zote majengo yake ni ya zamani sana na mengi yakiwa ni yale yalioachwa na mkoloni. Kati ya Mahakama za Mwanzo tisa zilizopo, majengo ambayo angalau yana hali nzuri ni matatu tu, ya Nandembo, Mlingoti na Ndesa. Mengine yaliyosalia yakiwemo ya Matemanga na Nakapanya ni chakavu sana, hayafai kukarabati na hivyo yamepangwa kujengwa upya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa ujenzi wa mahakama, Mahakama ya Mwanzo Nakapanya na Mahakama ya Wilaya ya Tunduru zimepangwa kujengwa mwaka 2019/2020 kulingana na upatikanaji wa fedha.