Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 11 Finance and Planning Ofisi ya Rais TAMISEMI. 84 2016-05-03

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:-
Ileje iliwahi kuwa katika Wilaya zilizoongoza kwa ufaulu wa wanafunzi, lakini miaka ya hivi karibuni ufaulu umeshuka na hii ni kutokana na miundombinu mibovu ya mazingira ya kufundishia:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa inaboresha miundombinu yote muhimu kwa utoaji wa elimu?
(b) Je, Serikali iko tayari kujaza pengo la Walimu liliko hivi sasa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janet Zebedayo Mbene, Mbunge wa Ileje, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuboresha miundombinu ya shule, Halmashauri ya Wilaya ya Ileje katika mwaka wa fedha 2015/2016, ilitengewa shilingi milioni 798.0 ambazo zilipokelewa kwa ajili ya ukarabati, ujenzi na umaliziaji wa miundombinu ya shule nne za Msomba, Luswisi, Itale na Bupigu. Vile vile, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, Halmashauri imetengewa shilingi milioni 130.8 ili kuendelea na uboreshaji wa mindombinu ya shule ya sekondari ya Ngulilo. Aidha, kupitia mapato yake ya ndani Halmashauri imetenga shilingi milioni 60.0 kwa ajili ya ukarabati wa nyumba za Walimu, ukarabati wa vyumba vya madarasa, ujenzi wa matundu ya vyoo na matengenezo ya madawati. Jitihada hizi zinakusudia kuinua kiwango cha elimu inayotolewa kwa wanafunzi katika Wilaya ya Ileje.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, mahitaji ya Walimu wa shule za msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje ni 819, waliopo sasa ni Walimu 567 na upungufu ni 252. Kwa upande wa shule za sekondari mahitaji ya Walimu wa sayansi na hisabati ni 156, waliopo ni 61 na upungufu ni 95. Hata hivyo, Wilaya ina zaidi ya Walimu wa masomo ya sanaa 105. Ili kuziba pengo la Walimu katika Halmashauri hiyo, Serikali imepanga kuajiri Walimu 35,411 waliohitimu kuanzia mwaka 2013/2014 na miaka ya nyuma ambapo sehemu ya Walimu hao watapangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje.