Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2018-09-05

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:-
Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nzasa – Kilungule – Buza – Temeke:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hiyo muhimu kwa wakazi wa Mbagala, Mwanagati na Temeke?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nasoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Nzasa – Kilungule – Buza – Temeke ina urefu wa kilomita 7.6. Barabara hii imeongezwa kwenye mpango wa maboresho ya Jiji ya Dar es Salam kupitia mradi wa DMDP na katika awamu inayofuata itajengwa kwa kiwango cha lami. Serikali imekwishalipa fidia ya jumla ya shilingi bilioni 3.25 kwa wananchi 310 ambao wanatakiwa kupisha mradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya usanifu imeshakamilika na kazi zinazotekelezwa ni ujenzi wa barabara ya lami kilomita 7.6, ujenzi, wa madaraja mawili yenye urefu wa mita 60 na makalvati makubwa matano kwenye bonde la Mto Mzinga, uwekaji wa taa barabarani jumla ya taa 324 ambazo zinatumia mwanga wa jua; pia kujenga vituo tisa vya mabasi ya daladala. Gharama ya kutengeneza shughuli hii inakadiriwa kuwa shilingi bilioni 22.6.