Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 58 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 494 2018-06-26

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE (K.n.y. MARY D. MURO) aliuliza:-
Kumekuwepo na mkanganyiko wa watumishi wa zimamoto kwenye viwanja vya ndege na viwanja hivyo kutokuwa huru katika kuwatumia kutokana na kuwa si sehemu ya waajiri wao:-
Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha viwanja vinajitegemea?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Deo Muro, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linasimamiwa na Sheria Namba 14, Sura ya 427 ya Mwaka 2007 iliyounganishwa Vikosi vya Zimamoto vilivyokuwa chini ya TAMISEMI na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kuwa chini ya Kamandi moja ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ni Taasisi za Serikali ambazo hufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kutoa huduma ya kulinda mipaka ya nchi, hivyo hakuna mkanganyiko wowote wa kiutendaji. Hata hivyo, naomba kulihakikishia Bunge lako Tukufu kuwa upo ushirikiano mzuri kati ya vyombo hivi vya ulinzi na usalama na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege katika kutekeleza majukumu yao.