Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 489 2018-06-26

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-
Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Kilwa:-
Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro huo ili kuleta amani katika Wilaya hizo kabla amani haijatoweka?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kilwa ilianzishwa kwa Tangazo la Serikali Na. 91 la tarehe 16 Mei, 1947 na Wilaya ya Liwale ilianzishwa kwa Tangazo la Serikali Na.185 la tarehe 5 Desemba, 1980. Hadi hapo hakukuwa na mgogoro wowote. Tangazo la Serikali Na. 134 la mwaka 1983 lilianzisha Halmashauri za Wilaya ambapo Mirui iliorodheshwa kama kata na kijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale na haikutajwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa.
Mheshimiwa Spika, Serikali inautambua mgogoro huo unaohusu mkanganyiko ulioko kati ya Kitongoji cha Mirui katika Kijiji cha Nanjirinji A, Kata ya Nanjirinji, Wilayani Kilwa kwa upande mmoja na Kijiji cha Mirui katika Kata ya Mirui Wilayani Liwale kwa upande wa pili.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mgogoro huo ni sehemu ya migogoro mingi inayoshughulikiwa na Serikali chini ya uratibu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nashauri Mbunge na wananchi wa maeneo husika wawe na subira wakati huu ambapo Serikali imetuma wataalam kwenye eneo hilo la mgogoro wanaofanya mapitio ya kina ya matangazo ya kuanzisha wilaya zote mbili na tangazo la kuanzisha halmashauri zote mbili kwa lengo la kuhakikisha mgogoro huo unapatiwa ufumbuzi wa kudumu ndani ya mwaka 2018/2019.