Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 488 2018-06-26

Name

Hassan Selemani Kaunje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S.
KAUNJE) aliuliza:-
(a) Je, ni lini Serikali itadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge?
(b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/ mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, utaratibu wa Halmashauri na Bunge kudhamini mikopo kwa Waheshimiwa Madiwani na Waheshimiwa Wabunge umetokana na kuwepo kwa utayari wa benki zinazokopesha mikopo hiyo, hususan NMB na CRDB ambazo baada ya kuonesha utayari, makubaliano maalum husainiwa ambayo ndiyo hutoa mwongozo wa namna mikopo itakavyotolewa pamoja na viwango vyake.
Mheshimiwa Spika, utaratibu wa aina hiyo hadi sasa haujawezekana kwa Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Mitaa na Vitongoji kwa kuwa hadi sasa hakuna benki iliyoonesha utayari wa kutoa mikopo ya aina hiyo. Hata hivyo, ipo fursa kwa kiongozi mmoja mmoja kuwasiliana na benki moja kwa moja kwa ajili ya makubaliano binafsi ya mkopo kulingana na kiwango cha amana alichonacho, thamani ya ardhi, nyumba anayomiliki au biashara.
(b) Mheshimiwa Spika, kwa kutambua kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Vitongoji na Mitaa kupitia Mpango wa Maboresho ya Serikali za Mitaa, Serikali ilitoa mwongozo kuwa viongozi hao wawe wanalipwa posho inayotokana na asilimia 20 ya mapato ya ndani ambayo hurejeshwa na Halmashauri kwenye Kijiji/Mtaa husika.
Mheshimiwa Spika, changamoto zilizopo za ukusanyaji hafifu wa mapato ya ndani zimekuwa zikisababisha ugumu wa kutekeleza mwongozo huo katika baadhi ya maeneo. Kwa sababu hiyo, Halmashauri zote zimeagizwa zifanye mapitio ya vyanzo vyote vya mapato na ziimarishe makusanyo ya ndani ili ziwe na uwezo wa kulipa posho hizo.