Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 487 2018-06-26

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:-
Hospitali ya Mtakatifu Gaspar imekuwa Hospitali ya Rufaa tangu mwaka 2011 na inahudumia wananchi wa Mikoa ya Tabora, Singida na Mbeya. Wakati wa kampeni mwaka 2015, Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kuipatia vifaa tiba, dawa na watumishi wa kutosha ili kupunguza changamoto wanazokutana nazo wagonjwa:-
Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa ili kusaidia hospitali hiyo kutoa huduma za afya kwa ufanisi na kuokoa maisha ya wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aisharose Ndogholi Matembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika kuboresha ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) katika utoaji wa huduma za afya, Serikali inatoa ruzuku ya fedha kwa ajili ya kulipia mishahara ya watumishi pamoja na ruzuku ya dawa na vifaa tiba. Jumla ya watumishi 50 wa Hospitali ya Mtakatifu Gaspar wanalipwa mishahara na Serikali ambapo ni Daktari Bingwa mmoja (Bingwa wa Upasuaji), Daktari mmoja, Daktari Wasaidizi (AMO) wawili, Tabibu wawili, Wauguzi 43 na Mteknolojia wa Maabara mmoja.
Mheshimiwa Spika, mgao wa dawa na vifaa tiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD) unaendelea kutolewa na Serikali katika Hospitali ya Mtakatifu Gaspar ambapo katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali ilitoa dawa zenye thamani ya shilingi milioni 105.67 na mwaka wa fedha wa 2017/2018 dawa zenye thamani ya shilingi milioni 114.67 zimetolewa katika hospitali hiyo. Aidha, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaandaa mwongozo wa gharama za matibabu katika hospitali ambazo siyo za Serikali ili kuzifanya hospitali hizo kutoa huduma zenye gharama nafuu.