Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 10 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 81 2016-05-02

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED aliuliza:-
Kituo cha Polisi cha Marine Kipili, hakina usafiri wa nchi kavu:-
(a) Je, ni lini Serikali itakisaidia kitu hicho usafiri wa nchi kavu angalau hata kukipatia pikipiki?
(b) Je, ni lini Serikali itaongeza mgao wa petroli?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally KeissyMohamed, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b), kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi Karibuni Serikali imegawa vyombo vya usafiri takribani kwa Wilaya zote, ikiwemo Wilaya ya Nkasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi Kipili kimo ndani ya Wilaya ya Nkasi kikihudumiwa na gari Namba PT 3836 ambayo ni jipya lililotolewa hivi karibuni. Hata hivyo, utaratibu utafanyika ili wapewe pikipiki iweze kusaidia kupunguza tatizo la usafiri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaongeza mgawo wa mafuta kulingana na hali ya uchumi itakavyoimarika.