Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 32 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 275 2018-05-18

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:-
TEHAMA imekuwa kichocheo cha maendeleo na hivyo kurahisisha ulipaji wa gharama (bills) mbalimbali kupitia miamala kwa njia ya simu. Mathalani, muda wa maongezi, ving’amuzi, umeme, kodi na laini mbalimbali.
Je, mlipaji aweke ushahidi wa aina gani katika kumbukumbu ngumu (hard paper) ili wakaguzi wa TRA waone au TRA itaridhika kwa kumbukumbu ya muamala?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango napenda kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa matakwa ya kifungu cha 35(1)(2), cha Sheria ya Usimamizi wa kodi ya mwaka 2015, kila mlipa kodi au mtu yeyote anayetakiwa kulipa kodi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatakiwa kutunza kumbukumbu za miamala katika mfumo wa kumbukumbu ngumu au mfumo wa kielektroniki. Aidha, kifungu cha 35(3) kinamtaka mlipa kodi kutunza kumbukumbu zake kwa muda wa miaka mitano kuanzia tarehe ambayo muamala umefanya au kwa muda zaidi kulingana na matakwa ya sheria.
Mheshimiwa Spika, sambamba na Sheria ya Usimamizi wa Kodi kifungu cha 69(3)(b) cha Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (The Value Added Tax Act, 2014) kinamtaka mlipa kodi aliyesajiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania katika mfumo wa malipo ya Kodi ya Ongezeko la Thamani kuwa na risiti ya EFD au ankara ya kodi (tax invoice) wakati akiwasilisha taarifa zake za mwezi (VAT return).