Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 268 2018-05-18

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:-
Mheshimiwa Rais katika Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 aliahidi kujenga kilometa 10 za barabara ya lami katika Manispaa ya Moshi.
(a) Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?
(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kusaidia Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kujenga mitaro katika barabara zake za lami ili kuzifanya zidumu muda mrefu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napensa kujibu swali la Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, Mbunge wa Moshi, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli, barabara zenye urefu wa kilometa 16.57 zimejengwa katika Manispaa ya Moshi kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2016 hadi Machi, 2018 ambapo kati ya hizo kilometa 6.06 zimejengwa kupitia fedha za Mfuko wa Barabara kwa gharama ya shilingi 2,076,497,094 na kilometa 10.51 zimejengwa kwa mkopo kutoka Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Kuimarisha Miji 18 (ULGSP) kwa gharama ya shilingi 8,384,872,640.87. Vilevile katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri inaendelea na ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilometa 2.79 kwa kiwango cha lami kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara unaotarajiwa kugharimu jumla ya shilingi 1,178,201,860.
Mheshimiwa Spika, kupitia Mradi wa Kuimarisha Miji 18 (ULGSP) katika kipindi cha Julai, 2016 hadi Machi, 2018 Serikali imejenga mitaro ya maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 11.57 kwa gharama ya shilingi 1,833,520,330. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imepanga kujenga mitaro ya maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 9.47 na mradi huu utagharimu jumla ya shilingi 1,612,952,130 kupitia fedha za Mfuko wa Barabara, ujenzi huu upo katika hatua za awali.