Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 28 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 235 2018-05-14

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:-
Tanzania haijaidhinisha na kujiunga rasmi na mkataba wa kupambana na silaha za sumu (Biological Weapons Convention):-
(i) Je, kwa nini Tanzania haijajiunga na mkataba huo?
(ii) Je, Serikali inafahamu madhara ya kutoidhinisha rasmi mkataba huo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ilisaini Mkataba wa Kupambana na Silaha za Baiolojia na Sumu tarehe 1 Agosti, 1972, lakini mpaka sasa haijaridhia mkataba huo. Kutoridhiwa kwa mkataba huo kulitokana na kutoonekana athari zake za moja kwa moja kwa wakati huo ambapo matumizi salama ya mkataba ikiwemo utafiti wa magojwa ya binadamu, wanyama na mimea yameendelea kufanyika nje ya mkataba huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto zinatokana na matishio mbalimbali ikiwemo ugaidi, zimesababisha hitajio la kuridhiwa kwa mkataba huo na kutekelezwa kwa vitendo baada ya kutungiwa sheria. Kutokana na umuhimu wa suala hili, Rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya kuridhia mkataba huo imeandaliwa na baada ya kupitia ngazi mbalimbali za maamuzi, azimio litaandaliwa kwa kuwasilishwa katika Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kuridhiwa.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inafahamu madhara yaliyopo hivi sasa ya kutoridhiwa kwa mkataba huo. Baadhi ya madhara hayo ni kama ifuatavyo:-
Kwanza, Tanzania kuwa katika kundi dogo la nchi ambazo hazijaridhia mkataba huo kama vile Haiti, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Misri, Somalia na Syria. Tanzania kuwepo katika kundi hili hakutoi taswira nzuri kwa Jumuiya ya Kimataifa kwani kati ya nchi hizo nyingi zina migogoro ya muda mrefu ya ndani.
Pili, kunanyima fursa kwa wataalam wetu kupata mafunzo mbalimbali yanayotolewa katika kujenga uwezo na kukabiliana na athari za mashambulizi ya silaha sumu na kibaiolojia.
Tatu, kunanyima fursa kwa wataalam na viongozi wa Kitanzania kushiriki kwenye uongozi wa taasisi mbalimbali za kimataifa zinasimamia sheria za silaha za kibaiolojia na sumu.
Nne, kunakosesha Serikali kutoa haki za msingi kupitia mahakama kwa makosa mbalimbali yanayoweza kufanywa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.