Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 232 2018-05-14

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-
Jimbo la Mpwapwa lina tarafa mbili, yaani Tarafa ya Mpwapwa na Tarafa ya Mima, lakini tangu kuanzishwa kwa Tarafa ya Mima hakuna miundombinu yoyote iliyojengwa kama vile Ofisi ya Tarafa na vyumba vya watumishi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Ofisi ya Afisa Tarafa na za watendaji wengine wa ngazi ya tarafa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Afisa Tarafa wa Tarafa ya Mima hajajengewa ofisi, anatumia Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Mima kutekeleza majukumu yake. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imetenga Sh.50,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Afisa Tarafa huyo itakayojengwa katika Kijiji cha Mima.