Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 230 2018-05-14

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Uyui inajulikana kwa jina la zamani la Tabora District Council (TDC) jina ambalo linagongana na jina la Manispaa ya Tabora (Tabora Minicipality). Wilaya kupitia Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa alileta maombi ya kubadili jina la Halmashauri kutoka Tabora District Council (TDC) na kuwa Halmashauri ya Uyui na Halmashauri imeomba kubadili jina la Jimbo la Tabora Kaskazini na Jimbo la uyui ikibeba jina la Wilaya na jina la eneo la kijiografia Uyui kwa sababu, hakuna tena Tabora Kaskazini, Kusini wala Magharibi:-
(a) Je, ni lini jina la Halmashauri litabadilishwa kuwa Halmashauri ya Uyui?
(b) Je, ni lini Jimbo la Tabora Kaskazini litaitwa Jimbo la Uyui?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Maige, naomba kwanza dakika moja tu nielezee furaha yangu; leo nimeamka saa 10:00 usiku kwa ajili ya kujiandaa kuja kujibu maswali, lakini furaha yangu kubwa ni kwa sababu Simba Sports Club baada ya kupata ubingwa sasa naamini Watanzania watapata wawakilishi kwenye michezo ya kimataifa ambao hawatatupa pressure kwa sababu vijana hawa wanajua kucheza vizuri sana mpira wa miguu, ahsante sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa baada ya maelezo hayo…
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge a Tabora Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mhesimiwa Mwenyekiti, maombi yenye mapendekezo ya kubadili jina la Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui sawa sawa na jina la Wilaya ya Uyui ambayo yamepitishwa na vikao vya kisheria vya Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Kamati ya Ushauri ya Mkoa yameshapokelewa na yako katika hatua za kupata ridhaa. Nawaomba wadau wote wa suala hili wawe na subira wakati Serikali inapomalizia mchakato huo.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Ibara ya 75 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mapendekezo ya kubadili jina la jimbo yaliyoridhiwa na baraza, wilaya na mkoa yanatakiwa kuwasilishwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo ndio yenye mamlaka ya uamuzi. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.