Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 77 2016-05-02

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:-
Umeme katika Mji wa Korogwe uliingia miaka 50 iliyopita ukitokea kwenye mitambo ya kuzalisha umeme iliyopo Mji wa Hale kilometa 30 toka Mji wa Korogwe. Umeme huo ulikusudiwa kupelekwa kwenye mashamba makubwa ya mkonge na chai na ili kuupata umeme huo kwa Mji huo ilibidi upite kwenye mashamba ya mkonge Magunda, Kwashemshi na kwenda kwenye mashamba ya chai ya Ambangulu na Dindira:-
Je, Serikali haioni ni wakati muafaka Mji wa Korogwe na viunga vyake kuunganishwa na Gridi ya Taifa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Chatanda, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hadi sasa Mji wa Korogwe hupata umeme kutoka kituo cha kuzalisha umeme cha Hale kilichounganishwa katika Gridi ya Taifa. Viunga vya Mji wa Korogwe navyo vimeunganishwa kwenye Gridi ya Taifa na hivyo vitaendelea kupata umeme kutoka katika vyanzo vya maji vya Hale. Mji wa Korogwe una maeneo ambayo pia bado hayajapata huduma ya umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya ni pamoja na Vitongoji vya Bagamoyo, Habitat, Kilole Sobibo, Kitopeni, Kwandungwe, Makwei, Ruengera Relini, Ruengera Darajani na baadhi ya maeneo ya vitongoji vya Mtonga, Kwamkole pamoja na Kwasemangube. Maeneo haya yataingizwa katika mpango wa utekelezaji wa bajeti ya TANESCO kwa mwaka 2017/2018.