Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 25 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 207 2018-05-09

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:-
Wilaya ya Itilima na Busega ni Wilaya mpya na hazina Hospitali za Wilaya.
Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya kwenye Wilaya hizo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri za Wilaya ya Itilima na Busega zilianzishwa mwaka 2015 na zina idadi ya watu 346,170 kwa Itilima na 224,527 kwa Busega. Ni kweli kwamba Halmashauri hizi bado hazina Hospitali za Wilaya na wananchi wanapata huduma kupitia zahanati 45 na vituo vya afya saba ambapo kati ya hivyo zahanati 27 na vituo vya afya vitatu vipo Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na zahanati 18 na vituo vya afya vinne vipo Halmashauri ya Wilaya ya Busega.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mpango wa maboresho na uimarishaji wa huduma za afya kwa kushirikiana na wadau (Canada na UNFPA), Serikali imepeleka kiasi cha shilingi bilioni 1.215 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya vituo vya afya. Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 525 ni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika Kituo cha Afya Ikilindo kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na shilingi milioni 450 ni kwa ajili ya Kituo cha Afya Nasa katika Halmashauri ya Wilaya Busega. Shilingi milioni 240 ni kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya zahanati nane ambapo kila zahanati imepatiwa shilingi milioni 30; zahanati hizo ni Gaswa, Mahembe, Migato na Nangale zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na Badugu, Nayamikoma, Ngasamo na Kikoleni zilizopo Halmashauri ya Wilaya za Busega.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri za Wilaya ya Itilima na Busega zimetengewa shilingi bilioni 1.5 kila moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali za Wilaya.