Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 16 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 134 2018-04-24

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K.n.y. MHE. PHILIPO A. MULUGO) aliuliza:-
Wilaya ya Songwe ina jumla ya vijiji 43 lakini mpaka sasa hakuna kijiji hata kimoja chenye umeme kwa mpango wa umeme wa REA toka awamu ya kwanza na ya pili:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inatoa upendeleo maalum kwa vijiji vya wilaya hii mpya katika awamu ya tatu ya REA?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Philipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Songwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Jimbo la Songwe lina jumla ya vijiji 43 ambapo kati ya vijiji hivyo, sita vilipatiwa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya kwanza na Vijiji 14 vya Ilasilo, Galula, Kanga, Mbala, Iseche, Majengo, Tete, Ifenkenya, Nahalyongo, Chang’ombe, Ifuko, Maamba, Songambele, Totowe na Mbuyuni vilipatiwa umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Pili.
Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Itiziro, Undinde, Mbangala, CHUDECO, Kambarage, Ilasilo, Kaloleni, Ndanga na Mwagala ni miongoni mwa vijiji 14 vinavyotarajiwa kunufaika na utekelezaji wa mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Julai, 2017 ambapo Mkandarasi M/S STEG International Services alipewa kazi za mradi katika Mkoa wa Songwe. Kazi zinazofanyika kwa sasa ni pamoja na kuleta vifaa katika maeneo ya mradi. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2019.
Mheshimiwa Spika, wigo wa mradi katika Jimbo la Songwe unajumuisha ujenzi wa kilometa 46.64 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 na kilometa 52.09 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4, ufungaji wa transforma 14 na kuunganisha wateja wa awali 3,980. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 13.05.
Mheshimiwa Spika, vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa pili unaotarajiwa kuanza kutekelezwa mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021. Mheshimiwa Spika, ahsante.