Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 125 2018-04-24

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL aliuliza:-
Kata ya Sigino na Vijiji vyake vyote katika Jimbo la Babati Mjini haina kabisa maji safi na salama:-
Je, ni nini mkakati wa Serikali wa kuipatia maji safi na salama Kata hiyo pamoja na Vijiji vyake?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pauline Philip Gekul, Mbunge wa Babati Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba vijiji vyote vinne katika Kata ya Sigino ndani ya Halmashauri ya Mji wa Babati vyenye wakazi 11,895 havina huduma ya maji safi na salama. Hata hivyo ziko hatua mahsusi zinazoendele. Mnamo tarehe 29 Mei, 2017, Halmashauri ya Mji wa Babati ilisaini mkataba wa Sh.487,470,000 kujenga mradi wa maji katika Kijiji cha Imbilili ambao ulipangwa kukamilika tarehe 30 Juni, 2018 lakini Mkandarasi Black Lion Limited amebainika kuwa na uwezo mdogo kwani hadi sasa ametekeleza kazi kwa asilimia saba tu. Naishauri Halmashauri ambapo Mheshimiwa Pauline Gekul ni Diwani, itathmini haraka hali hiyo na ichukue hatua haraka kwa manufaa ya wananchi.
Mheshimiwa Spika, hatua nyingine kubwa inayoendela ni utekelezaji wa mkataba kati ya Halmashauri na Mkandarasi Maswi Drilling Company Limited kuchimba visima virefu katika Vijiji vya Sigino, Singu na Haraa kwa shilingi milioni 94.5 ambao umefikia asilimia 25 na utakamilika tarehe 30 Juni, 2018. Usanifu na ulazaji wa mabomba yakayosambaza huduma za maji safi na salama kwa wananchi utaanza mwaka 2018/2019 kwa kutumia Sh.611,137,000 ambazo zimetengwa kutekeleza mradi huo. Ahsante.