Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 15 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 120 2018-04-23

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-
Mradi wa umeme wa 400KV kutoka Kinyerezi hadi Arusha umepita maeneo mengi ya nchi yetu ikiwa ni pamoja na Jimbo la Kibaha Mjini, uthamini wa mali za waathirika ulishafanyika toka mwaka 2015.
Je, Serikali itawalipa lini wananchi hawa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshiiwa Mwenyekityi, Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Kinyerezi hadi Arusha. Mradi huu unahusisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovolti 400 yenye urefu wa kilometa 664 pamoja na kilometa 40 kutoka Kibaha hadi Zinga na kilometa 60 kutoka Segera hadi Kange - Tanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu pia unahusisha ujenzi wa vituo vya kupoza umeme vya Chalinze, Segera, Kange, Tanga na Zinga Bagamoyo. Mradi huu utejengwa kwa mkopo kutoka Benki ya Exim ya China.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 kazi ya uthamini wa mali za wananchi kutoka Kibaha hadi Chalinze ilifanyika ili waweze kulipwa fidia na kupisha ujenzi wa mradi. Kazi inayofanyika kwa sasa ni kukamilisha taratibu za maandalizi ya malipo kwa wananchi waliohakikiwa kwa ajili ya malipo ya fidia. Zaidi ya shilingi bilioni 21.56 zimetengwa na Serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wanaopitiwa na mradi katika maeneo ya Kisarawe, Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Bagamoyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa wataanza kulipwa fidia baada ya uhakiki wa madai ya fidia hiyo kukamilika. (Makofi)