Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 87 2018-04-17

Name

Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:-
Serikali ilitoa shilingi milioni 300 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Namanyere Makao Makuu ya Wilaya ya Nkasi hadi Ninde yenye urefu wa kilometa 40 lakini hadi sasa ujenzi wa barabara hiyo bado haujakamilika kwa muda mrefu sasa.
(a) Je, ni lini Serikali itachukua hatua kwa kufuatilia na kuchunguza matumizi ya fedha zilizotolewa na kuchukua hatua ili ujenzi wa barabara hiyo uweze kukamilika?
(b) Je, ni lini wananchi wa Ninde wataondokana na changamoto ya barabara?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Silafu Jumbe Maufi, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, barabara ya Namanyere - Ninde yenye urefu wa kilomita 60 katika mwaka wa fedha 2014/2015 ilitengewa shilingi milioni 350 za kufanyia matengenezo kama ifuatavyo:-
• Ujenzi wa daraja moja lenye urefu wa mita 20 kwenye Mto Lwafi kwa shilingi milioni 73.69;
• Ujenzi wa daraja moja lenye urefu wa mita 50 kwenye Mto Ninde kwa shilingi milioni 33.922 ;
• Ujenzi wa madaraja mawili yenye urefu wa mita tano kila moja kwenye msitu wa Lwafi kwa shilingi milioni 26.65; na
• Kuifungua sehemu iliyokuwa imebakia ya barabara ya urefu wa kilometa 25 kwa kufanya matengenezo kwa kiwango cha udongo na kujenga makalvati mistari 15 kwa shilingi milioni 154.735 pamoja na gharama za usimamizi jumla ya shilingi milioni 61.003.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kupambana na changamoto ya barabara kwa wananchi wa Ninde kwa kuitengea fedha za matengenezo barabara hiyo. Katika mwaka wa fedha 2015/2016 shilingi milioni 44.58 zilitengwa kwa ajili ya kufanyia matengenezo ya muda maalum kwa urefu wa kilometa mbili. Aidha, mwaka wa fedha 2016/2017 shilingi milioni 20 zilitengwa na kutumika kuimarisha sehemu korofi zenye urefu wa mita 500.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kufanyia matengenezo barabara hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha ili iweze kupitika na kuondoa tatizo la usafiri kwa wananchi wa Ninde na maeneo jirani.