Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 11 | Sitting 8 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 67 | 2018-04-12 |
Name
Margaret Simwanza Sitta
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Urambo
Primary Question
MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-
Pamoja na kuishukuru Serikali kwa hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kumwondolea mkulima matatizo ya zao la tumbaku:-
• Je, Serikali imechukua hatua zipi katika kuimarisha utendaji kazi wa Bodi mpya ya Tumbaku ili ifanye kazi kikamilifu?
• Je, Serikali inawahakikishiaje wakulima wa tumbaku upatikanaji wa mbolea kwa wakati?
Name
Dr. Mary Machuche Mwanjelwa
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mbeya Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania ilizinduliwa rasmi tarehe Mosi Disemba, 2017. Ili kuimarisha utendaji kazi wake kikamilifu, Serikali imeiagiza kuwa tumbaku iendelee kuwa miongozi mwa mazao mkuu yanayowanufaisha wakulima ili kuliingizia Taifa fedha za kigeni kwa kuhakikisha kuwa ubora wa tumbaku unaongezeka kwa asilimia 15 ifikapo mwaka 2021 na uzalishaji wake kufikia tani laki moja na ishirini kutoka tani elfu sitini na tatu za sasa.
Mheshimiwa Spika, tumbaku inazalishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu na wakulima wanazalisha kwa mkataba ili kuwa na soko la uhakika.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tumbaku ni moja ya zao la kimkakati, Bodi imelekezwa kuyataka makampuni ya ununuzi kufanga mikataba na Bodi ya Tumbaku Tanzania na kisha kuyapangia maeneo ya kwenda kununua badala ya utaratibu wa sasa ambapo makampuni hujichagulia maeneo ya kwenda kununua.
Mheshimiwa Spika, hatua nyingine ni kutafiti na kubaini aina nzuri za tumbaku zinazopendwa na wanunuzi ili zilimwe na kuwauzia wanunuzi wa aina hizo za tumbaku; kuwachukulia hatua za kinidhani watendaji wasiowajibika kikamilifu na kufuata vizuri kalenda ya uzalishaji wa tumbaku.
(b) Mheshimiwa Spika, katika msimu wa mwaka wa 2017/2018, mbolea ya tumbaku ilichelewa kutokana na kuchelewa kwa maafikiano ya bei ya kununulia tumbaku ambayo ni kigezo kwa kila kampuni kuahidi kiasi cha tumbaku itakachonunua na hivyo kubaini kiasi cha mbolea itakayotumika kuzalisha kiasi hicho cha tumbaku.
Mheshimiwa Spika, ili mbolea ianze kuagizwa maafikiano ya bei yanatakiwa kukamilika kati ya Machi na Mei kila mwaka. Katika msimu wa kilimo wa 2018/2019, Bodi ya Tumbaku Tanzania inaendelea kuratibu majadiliano ya bei kati ya wanunuzi na wakulima ili uagizaji wa mbolea ufanyike mapema. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved