Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 40 2018-04-09

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:-
• Je, Serikali inatumia pesa kiasi gani kuhudumia mfungwa mmoja kwa siku kwa huduma ya chakula tu?
• Vitendo kama kulala chini, kulala bila blanketi au shuka, kulala bila neti vimekuwa vya kawaida kabisa katika Magereza yetu nchini; je, hii nayo ni sehemu ya adhabu ambayo wafungwa wanapewa kwa mujibu wa sheria?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Jeshi la Magereza katika kutekeleza jukumu lake la kuwapokea na kuwahifadhi wahalifu kisheria, pia hutoa huduma ya chakula kwa wahalifu kupitia bajeti inayotengwa na Serikali kila mwaka wa fedha. Gharama ya chakula kwa mfungwa mmoja kwa siku ni wastani wa shilingi 1,342.
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma za wafungwa na mahabusu Magerezani kwa kununua vifaa mbalimbali vya malazi ikiwemo magodoro, shuka, mablanketi na madawa ya kuua wadudu kwa awamu kadri ya upatikanaji wa fedha. Kwa msingi huo inapotokea ukosefu wa huduma hizo, inakuwa siyo sehemu ya adhabu kwa wafungwa bali hutokea kutokana na idadi kubwa ya wafungwa gerezani.