Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 57 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 468 2017-06-30

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:-
Walimu Wilayani Maswa wana uhaba wa nyumba za kuishi; pamoja na juhudi za wananchi kujenga nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari lakini walimu hao bado wanahitaji kujenga nyumba zao wenyewe za
kudumu.
Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu maalum wa kutoa mikopo kwa walimu hao ili wajenge nyumba zao binafsi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina uhitaji wa nyumba za walimu 1,358. Nyumba zilizopo ni 479 na hivyo upungufu ni nyumba 879.
Mheshimiwa Spika, kutokana na upungufu huu Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina mpango wa kujenga nyumba 16 katika mwaka wa fedha 2017/2018. Aidha, kati ya nyumba hizo, nyumba nane zitajengwa kwa bajeti ya 2017/2018 (CDG) na nyumba nyingine nane zitajengwa kwa kutumia mapato ya ndani y (own source) ya Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia kuwa tatizo la upungufu wa nyumba halitaweza kumalizwa na Serikali peke yake, Serikali inawashauri walimu wa Halmashauri ya Maswa na walimu wote nchini wanaohitaji kujenga nyumba zao binafsi kukopa fedha kutoka katika taasisi za fedha zinazokubalika Kisheria.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali inatoa wito kwa walimu nchini kote kujiunga na vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS) ili waweze kukopa kwa riba nafuu kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za binafsi. Pia Serikali inawashauri walimu kutumia mikopo ya nyumba inayotolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.