Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 55 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 459 2017-06-28

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatatua au kumaliza kabisa tatizo la baadhi ya wakazi wanaoitwa Wahamiaji katika Vijiji vya Nyabuzume, Tiring’ati, Nyaburundi na Bigegu ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakisumbuliwa na hoja hiyo bila kupewa ufumbuzi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Getere, Mbunge wa Bunda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama inavyofahamika nchi yetu, hususan maeneo ya mipakani, imekuwa na tatizo la wahamiaji ambao hufahamika kama walowezi walioingia na kuishi nchini kwa miaka mingi. Wahamiaj hawa waliingia nchini kwa sababu mbalimbali tangu wakati wa ukoloni, ikiwemo kufanya kazi katika mashamba na migodi ya wakoloni, vita vya kikabila na uhaba wa ardhi katika nchi zao na pia kuvutiwa na hali ya amani iliyopo katika nchi yetu. Kwa mujibu wa Sheria ya Uraia, Sura Namba 357, kama ilivyorejewa mwaka 2002 walowezi hawa hawatambuliwi kama raia wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge ni miongoni mwa maeneo yenye tatizo hili. Hivyo, kwa kutambua changamoto za tatizo hili Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji mwaka 2009 ilifanya sensa ya wahamiaji hao katika maeneo mbalimbali hapa nchini, ikiwa ni pamoja na vijiji tajwa ambapo, ilibaini kijiji cha Nyabuzume kuna walowezi 160, Tiring’ati 48, Nyaburundi 530 na Bigegu 72.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya sensa hiyo, Serikali imekuwa ikiwapatia wahamiaji hao vibali vya kuishi nchini baada ya kukidhi vigezo ili kuwatambua na kuhalalisha ukaazi wao.